Jeshi la Wananchi wa Tanzania (JWTZ) pamoja na Jeshi la Polisi zashiriki " 2nd Military All African Games"

Jeshi la Ulinzi wa Wananchi wa Tanzania (JWTZ) lashiriki mashindano ya  " 2nd Military All African Games" yanayofanyika katika jiji kuu la Abuja Nchini Nigeria,katika mashindano hayo JWTZ kushiriki jumla ya michezo mitatu ambayo ni GOLF,  BOXING & MARATHON, mashindano hayo yalianza tarehe 18 – 30th Nov 2024.

USHINDI KATIKA MARATHON

Alphonce Simbu amefanikiwa kuipeperusha vyema Bendera ya Tanzania kwa upande wa (JWTZ NGOME) kwa kushika nafasi ya Kwanza kupata MEDAL ya GOLD katika Mbio za KM 42 Marathon ya 2nd Military All African Games iliyofanyika Abuja Nigeria

Simbu alitumia muda wa saa 2:17.19 alifuatiwa na DedefiGelato wa Ethiopia aliyetumia saa 2:18.31 na Malgeria  Laamedi El Hadi alishika nafasi ya tatu kwa kutumia saa2:19.59.

Magdalena Shauri  amefanikiwa kuipeperusha vyema Bendera ya Tanzania kwa upande wa Wanawake (JWTZ NGOME) kwa kushika nafasi ya Kwanza kupata MEDAL ya GOLD katika Mbio za KM 42 Marathon ya 2nd Military All African Games iliyofanyika Abuja Nigeria

Magdalena alitumia muda wa saa 2:36.29 alifuatiwa na Cheptoyek Ruth na Chebet Emily wa Uganda waliomaliza nafasi ya Pili aliyetumia saa 2:41.07 na wa Tatu alitumia muda wa saa 2:44.10.

Transfora Mussa wa Kanda ya POLISI TANZANIA ameshika nafasi ya Kwanza upande wa Wanawake na kujinyakulia Medali ya GOLD katika  Mbio za Fulham KM 10 Uingereza

Alitumia dk 31:53 akivunja rekodi ya mshindi wa 2023 kutoka Kenya aliekimbia kwa muda wa dk 33;11 katika mshindano hayo ya Fulham Uingereza.

USHINDI KATIKA BOXING

Bondia wa JWTZ Yusuf Changalawe kushinda pambano kwa KO baada ya kumpiga Mnaigeria katika mashindano ya 2nd Military All African Games yaliyofanyika Abuja nchini Nigeria tarehe 19 Nov 2024.

Matukio katika picha

Mwenyekiti wa BAMMATA Brig Gen Saidi Hamis Said ( alievaa jezi nyeupe) pamoja na Wanamichezo na Viongozi

Mwenyekiti wa BAMMATA Brig Gen Saidi Hamis Said ( alievaa jezi nyeupe) pamoja na Wanamichezo na Viongozi

Mwanariadha Alphonce Simbu amefanikiwa kuipeperusha vyema Bendera ya Tanzania

Mwanariadha Alphonce Simbu amefanikiwa kuipeperusha vyema Bendera ya Tanzania

Magdalena Shauri  aipeperusha vyema Bendera ya Tanzania kwa upande wa Wanawake

Magdalena Shauri aipeperusha vyema Bendera ya Tanzania kwa upande wa Wanawake

Transfora Mussa wa Kanda ya POLISI TANZANIA ameshika nafasi ya Kwanza

Transfora Mussa wa Kanda ya POLISI TANZANIA ameshika nafasi ya Kwanza

Yusuf Changalawe ashinda pambano kwa KO

Yusuf Changalawe ashinda pambano kwa KO