Mashindano ya Majeshi (CISM) Wuhan China 2019

JWTZ yashiriki michezo ya CISM ikijumuisha  michezo ya mieleka, riadha na ngumi Wuhan China mwaka 2020.

1.    Timu Teule ya Mchezo wa Ngumi “Boxing”

Timu Teule ya Mchezo wa Ngumi ilishiriki Michezo ya Majeshi ya Dunia (CISM) iliyofanyika mjini Wuhan nchini China kuanzia tarehe 18 Oct 19 hadi tarehe 27 Oct 19 na matokeo yalikuwa ifuatavyo:-

Tarehe 18/10/19 timu ya ngumi ilianza kushiriki michezo hiyo kwa meneja na kocha kushiriki katika kikao (technical meeting) kupata maelekezo ya mashindano na kufanya “draw”. Michezo ilichezwa kwa mtoano.

a. Tarehe 19/10/19 mabondia wanne (4) wa Tanzania walipanda ulingoni kupeperusha bendera ya Tanzania kulingana na matokeo ya “draw’

b. Matokeo ya jumla Cpl Seleman Kidunda ameshika nafasi ya tano (5) katika uzito wa 75 Kg na kutunukiwa cheti cha ushindi.

c.   Sgt Burhani Abdallah alicheza dhidi ya Poppe (German). Matokeo Sgt Burhani alishindwa kwa Tush (KO).

d.  Cpl subiri Mwanzembe aliyecheza uzito wa 57 Kg (Free Style) peke yake alipata cheti cha ushindi wa nafasi ya tano.

e.  Sgt Burhani Abdallah alicheza dhidi ya Poppe (German). Matokeo Sgt Burhani alishindwa kwa Tush (KO).

f.    Cpl subiri Mwanzembe aliyecheza uzito wa 57 Kg (Free Style) peke yake alipata cheti cha ushindi wa nafasi ya tano.

2.    Timu Teule ya Riadha

Timu Teule ya Riadha ilishiriki Michezo ya Majeshi ya Dunia (CISM) iliyofanyika mjini Wuhan nchini China kuanzia tarehe 18 Oct 19 hadi tarehe 27 Oct 19 na matokeo yalikuwa ifuatavyo:-

a.  Track and  Field: Katika sehemu hii ya mchezo wa Riadha, mashindano yalifanyika kwa mujibu wa ratiba iliyotolewa mara baada ya kamati ya ufundi kuridhia.

(1)       Umabali 1500m: Tarehe 26 Oct 19, Mshiriki wetu Pte Cesilia Panga alishiriki mbio za fainali za 1500m (wanawake) na kushika nafasi ya 10 kati ya washiriki 21.

(2)       Umbali 10,000M: Tarehe 23 oct 19 saa 19:20 mbio za mita 10000 zilichezwa kama fainali bila kupita makundi (Elimination stage) JWTZ lilikua na washiriki wawili na  matokeo yao ni kama ifuatavyo:-

(a)       Pte Gisamoda  Giniki – Alishika nafasi ya nne kati ya washiriki 36 toka nchi mbalimbali.

(b)       SM Sylnester Marko – Alishika nafasi ya sita kati ya washiriki 36.

(3)    Umbali 5000M: Tarehe 24 Oct 19 saa 0930 washiriki wetu wawili walicheza hatua ya awali 5000m na kufanikiwa kupita hatua ya fainali. Hatua ya awali ilikuwa na jumla ya washiriki 40. Wachezaji wetu wawili wafuatao waliofaulu kuingia hatua na fainali ya wachezaji 15:-

(a)       Pte  Faraja  Damasi

(b)       Pte  Panga  Joseph.

Pte Faraja Damasi – alishika nafasi ya sita (6) katika mbio za mita 5,000 na Pte Panga Joseph – alishika nafasi ya nane (8) katika mbio za mita 5,000.

(4)   Marathon (42.195 Km): Mchezo wa pili kwa upande wa riadha ilihusisha mbio ndefu Full Marathon 42.195km mnamo TNS 270800C 0ct 19. Katika mchezo huo (Men’s individual Marathon):-

(a)   Pte Alphonce Simbu alipata nafasi ya pili (2) kati ya washiriki 97 waliokuwa kwenye orodha na washiriki 87 waliomaliza mbio hizo.

(b)     Mshiriki wa pili kwa upande wa marathon Cpl Ezekiel Ng’imba hakuweza kumaliza mbio kutokana na majeraha ya kisigino.

(c)      Mbio hizi Cpl Alphonce Simbu alipata Medali ya Fedha (Silver Medal) kwa kukimbia kwa muda wa 2:11:16, Mkuu wa Majeshi kwa niaba ya Jeshi alimpongeza kwa kupata matokeo hayo mazuri na kupandishwa cheo toka PTE na kuwa CPL. Pamoja na kupata medali ya Fedha (Silver) kupitia kwa Cpl Alphonce Simbu,

wachezaji wengine watano wa riadha walitunukiwa vyeti vya ushindi ifuatavyo:-

a.    Pte Gisamoda Giniki  alishika nafasi ya nne (4) katika mbio za mita 1000

b.    Servieman Sylivester Marko alishika nafasi ya sita (6) katika mbio za mita 1000

c.     Pte  Faraja  Damasi  alishika nafasi ya sita (6) katika mbio za mita 5000

d.    Pte Panga Joseph alishika nafasi ya nane (8) katika mbio za mita 5000

e.    Cpl Magdalena Shauri alishika nafasi ya nane katika mbio za mita 5000