Mwenyekiti wa BAMMATA Brig Gen Suleiman Gwaya ametoa wito kwa kanda mbalimbali zinazounda BAMMATA kuongeza timu za Ngumi, Mchezo wa Vishale na Judo katika michezo ya majeshi inayotarajiwa kufanyika jijini Mbeya baadaye mwaka huu.
Hayo ameyaongea siku ya tarehe 22 April 2022 katika kikao cha Kamati Tendaji iliyokaa katika ukumbi wa mikutano uliopo katika kikosi cha Makutupora JKT
Mwenyekiti na wajumbe wa BAMMATA wakiwa kwenye kikao
Kamati tendaji ya BAMMATA katika picha ya pamoja
Wajumbe wa BAMMATA kwenye kikao