Mwenyekiti wa BAMMATA amezitaka kanda za BAMMATA kuongeza timu katika michezo ya majeshi inayotarajiwa kufanyika jijini Mbeya mwaka huu
Mwenyekiti wa BAMMATA Brig Gen Suleiman Gwaya ametoa wito kwa kanda mbalimbali zinazounda BAMMATA kuongeza timu za Ngumi, Mchezo wa Vishale na Judo katika michezo ya majeshi inayotarajiwa kufanyika jijini Mbeya baadaye mwaka huu.